Mapambano ya urithi yanazidi kuchukua sura mpya! Ritha anamshawishi Ray amuunge mkono katika vita ya kupata mali za kaka yake, lakini upande wa pili Abby anamwonya Nelly kuhusu Ray — akisisitiza kuwa nia yake ni kisasi kwa kile kilichowatokea wazazi wake. Hali inazidi kuwa tete pale Ritha anapokutana uso kwa uso na Tima, mke wa kaka yake, kwenye mvutano mkali juu ya watoto na mali za familia. Ni nani atashinda hii vita ya mirathi? Usikose HUBA kwenye Maisha Magic Bongo!