channel logo dark
Jivu S1 SP BB
channel logo dark

Jivu

160DramaPG13
Jivu Season Poster

Telenovela Huchora mstari kati ya walionacho na wasio nacho ambapo kwa katika
jumba la kifahari la mwanamke mzee, mwenye uchungu na baridi (BARKE), mama wa watoto watatu anapata
katika mapambano ya kumlinda mwanae asiolewe na msichana anayetoka naye nje ya nchi
ambapo alienda kwa masomo yake, Munir na Karen wanakabiliwa na vikwazo vingi kutoka kwa BARKE
na wanafamilia wengine kwani inaaminika kuwa ni mwiko kwa Munir kuoa
msichana ambaye ni tofauti na mila na desturi zao… maisha katika jumba hili la kifahari huwa
kuzimu hai si kwa Karen pekee bali pia wahudumu wa nyumbani hasa Ajuaye Who
hutokea kubeba siri nyingi za familia

S1 | E14
09 Juni 13:30
'S1/E14'. Amanzi anaendelea kumtesa Chema. Karen anamfuma Zingizi nje mida ya usiku wa manane. Mtupe anaenda kwa Gumbo k...

Kali mpya ndani ya maisha magic bongo

News
07 Mei 2025
Tamthilia za Jivu na The Wife zimepokelewa vizuri tangu zilipoanza kuonyeshwa rasmi ndani ya Maisha Magic Bongo, watazamaji wamevutiwa nazo kutokana na kugusa maisha yao ya kawaida.
Season 1

Upendo, familia, na mapambano ya mila na desturi dhidi ya kizazi kipya vimewasilishwa vyema katika tamthilia mbili mpya: The Wife na Jivu. Tamthilia zote mbili zinabamba ndani ya Maisha Magic Bongo kwa kasi ya ajabu na kuwaacha watazamaji wakiwa na maswali na hisia mseto baada ya kila kipindi.

Mapenzi na Siri ya Familia ya Zulu – The Wife

Kutoka Afrika Kusini, The Wife ni tamthilia inayoangazia familia ya Zulu - ndugu wa damu ambao wamefungwa pamoja na upendo, uhalifu na nguvu za giza. Kila mmoja wao hupigana kulinda jina la familia, huku wake zao wakijaribu kukabiliana na misukosuko ya ndoa iliyojaa udanganyifu, uwongo, na mapambano ya ndani.

Tamthilia hii inatoa mchanganyiko wa hisia: mapenzi ya kweli, maumivu ya kuvunjika kwa uaminifu na mgongano wa maamuzi magumu. Ni hadithi inayoonyesha kwamba hata katika familia inayojaribu kujenga umoja, kuna migogoro ambayo inaweza kusambaratisha upendo na damu.

Upendo uliojaribiwa na mila kali- Jivu

Kutoka Tanzania, Jivu anasimulia hadithi ya Munir na Karen: Vijana  walioazimia kuoana. Changamoto yao kubwa? Mama mkali wa Munir ambaye anaamini Karen hafai kabisa kuwa mke wa mwanawe.

Hii inaakisi jamii nyingi za Kiafrika ambapo maamuzi ya ndoa bado yanategemea ridhaa ya wazazi, hasa akina mama. Jivu ni hadithi ya mapambano ya kizazi kipya kutafuta uhuru wa kuchagua upendo bila hofu ya hukumu kutoka kwa jamii au familia.

Ni hadithi ya mvutano kati ya moyo wa mwanadamu na sheria zisizoandikwa za jamii - upendo, heshima, maamuzi, na uhuru wa maisha.

Maonyesho yanayoakisi maisha ya wengi

Ingawa The Wife na Jivu zinatoka nchi tofauti, zote zinazingatia mapambano ya mtu binafsi dhidi ya familia au mfumo wa kijamii. Wanaeleza kwa kina jinsi upendo unavyoweza kustawi au kufifia katika mazingira ya mikazo ya kitamaduni na kiuchumi.

Kupitia wahusika, hadithi, na maudhui ya kina, tamthilia hizi mbili zimeleta upepo mpya kwenye televisheni na majukwaa ya kidijitali na zinaendelea kuwavutia watazamaji wa rika zote.

Usikose! Tazama The Wife na Jivu sasa kwenye Maisha Magic Bongo kwa burudani ya kiwango cha juu, iliyojaa utambulisho wa Kiafrika na mvuto halisi wa maisha.a